Bondia wa ngumi za kulipwa nchini
ambaye ni bingwa wa zamani wa Afrika Mashariki na Kati, Mada Maugo ‘Maugo Jr’,
amesema lazima atamuulia ulingoni mpinzani wake Thomas Mashali.
Maugo amesema, asipokufa Mashali, basi naye atafia ulingoni wakati wa tamasha hilo la Usiku wa Matumaini lililopangwa kufanyika Agosti 8 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
“Hivi ninavyozungumza nipo gym na kocha wangu ambaye
amewasili kutoka Nairobi ili kuendelea na maandalizi, cha muhimu ni kumuomba
Mungu niwe na afya njema mpaka siku ya ‘game’,” alisema Maugo kwa sauti ya
kujiamini.
Maugo na Mashali ni mabondia wenye
upinzani wa jadi ndani na nje ya ulingo ambapo watapanda ulingoni kurushiana
makonde katika kilele cha Usiku wa Tamasha la Matumaini linalotarajiwa
kufanyika Agosti 8, mwaka huu katika Uwanja wa Taifa jijini Dar.
0 COMMENTS:
Post a Comment