Vita ya maneno! Kauli inayofaa kutumika kwa
makocha wa Simba na Yanga ambao wamejibizana kuhusu kambi ya Visiwani Zanzibar.
Maximo, amesema kuwa kikosi chake
kitakuwa na kambi Kisiwani Pemba kwa ajili ya kujiandaa na michuano mbalimbali
inayowakabili ikiwemo ligi kuu itakayoanza kutimua vumbi Septemba 20.
Maximo alizitaja sababu hizo kuwa ni pamoja na hali ya hewa ya utulivu, uzuri
wa viwanja vyao na muda mfupi uliobakia kujipanga.
Alikwenda mbali na kufafanua kuwa kwa
muda huu, ingekuwa vigumu kuweka kambi mbali na Tanzania, hivyo ameamua kuomba
kambi karibu ili kufidia muda wa majaribio.
“Zanzibar kuna hali nzuri ya utulivu,
viwanja vizuri kwa mazoezi lakini pia unaweza kuangali muda pia tulionao wa
kujiandaa, nafdikiri ni suala la ‘kuofa’ muda wa mazoezi, badala ya kwenda
mbali na nyumbani,”alisema kocha huyo wa zamani wa timu ya taifa.
Hata hivyo alishindwa kutaja tarehe
maalumu ya kwenda Pemba, ambapo alisema itakuwa baada ya wachezaji wote walio
katika timu zao za taifa kurejea.
0 COMMENTS:
Post a Comment