September 30, 2014

MCREGGAN AKIKABIDHIWA MOJA YA KADI ZAKE ZA BIMA.....SHEMEJIIIII


Kundi maarufu la vichekesho nchini la The Original Comedy limepata mafanikio mengine baada ya benki ya CRDB kuwapa bima za aina mbili.

The Original Comedy chini ya kiongozi wao Sekioni David maarufu kama Seki wamepata bima ya maisha pia bima ya matibabu au unaweza kusema bima ya afya.
Kupitia kampuni yake mtoto ya CRDB Microfinance, benki ya CRDB imetoa bima ya matibabu kwa The Original Comedy  kupitia kampuni ya AAR.
BOSI WA COMEDY ORIGINAL, SEKI AKIELEZEA JAMBO

Lakini pia CRDB imetoa bima ya maisha kwa The Original Comedy kupitia kampuni ya African Life.
Shughuli nzima ya kukabidhiana kadi za bima hizo, ilifanyika leo kwenye Benki ya CRDB tawi la Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Wakati wa makabidhiano hayo, wasanii wa kundi hilo, Joti, Vengu, McRegan, Mpoki na kiongozi wao Seki walikuwa katika eneo hilo.
JOTI NAYE AKIPOKEA KADI YAKE YA BIMA...

Pamoja na wasanii hao kuwa kivutio, mmoja wa warembo waliowahi kung’ara katika Miss Tanzania, Nargis Mohammed ambaye ilielezwa ‘anapiga job’ kwenye kampuni ya CRDB Microfinance, naye alikuwa katika eneo hilo.


 “Mbali na kupata matibabu kwenye hosptali bora za hapa nchini lakini pia wana nafasi ya kutibiwa nje ya nchi kama vile Kenya, Afrika Kusini na India, hii siyo kwao pekee bali hata kwa familia zao.
“Tumeamua kufanya hivyo kutokana na kundi hili kuwa bora zaidi hapa nchini hivyo wadau wengi wakishaona hivyo ikiwa ni pamoja na makundi mengine basi watavutiwa na hali hiyo nao watataka kupata huduma hii,” alisema Arthur Mosha, Meneja wa kitengo cha Bima, CRDB.

Naye kiongozi wa kundi la The Original Comedy, Seki alisema kuwa wameipokea kwa mikono miwili huduma hiyo waliyopewa ambayo sasa imewapa amani katika maisha yao ya kila siku hivyo watafanya kazi yao bila ya kuwa na wasiwasi tena.
“Huduma hii pia imemuhusisha ndugu yetu Joseph Shamba ‘Vengu’ ambaye ni mgunjwa, ila yeye atapata bima ya maisha pekee na siyo ile ya matibabu.
“Anaweza kupata bima ya matibabu endapo hali yake ya kiafya itarejea kawaida kama zamani lakini kwa sasa imekuwa vigumu kutokana na sababu mbalimbali,” alisema Seki.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic