November 26, 2014


Wakati Simba wakiwa tayari wameanza mazoezi ya nguvu, kwa ajili ya mtanange mkali wa Nani Mtani Jembe 2 dhidi ya Yanga, kocha mkuu wa klabu hiyo, Mzambia, Patrick Phiri, anatarajia kutua nchini kesho Alhamisi.


Phiri, ambaye aliondoka nchini wiki iliyopita, anatarajiwa kurejea nchini kesho kwa ajili ya kuendelea kuiandaa timu hiyo.

Hata hivyo, wakati Phiri akitarajiwa kutua nchini kesho, Kocha wa Yanga, Marcio Maximo atashuka Bongo leo, akitokea kwao Brazili sambamba na kiungo mpya Emerson Roque ambaye atakuja kwa ajili ya majaribio.

Akizungumza na Championi Jumatano jana, Katibu Mkuu wa Simba, Stephene Ally, alisema kuwa Phiri anatarajia kutua nchini kesho, tayari kwa ajili ya kukiandaa kikosi chake kujiweka fiti kuelekea mchezo wa kukata na shoka dhidi ya watani wao wa jadi, Yanga utakaopigwa Desemba 13, mwaka huu.

“Kama hakutakuwa na matatizo yoyote, basi kocha atatua nchini keshokutwa (Alhamisi) kwa ajili ya kuendelea na majukumu yake, ikizingatiwa tuna mchezo mkubwa mbele yetu, hivyo anatakiwa kurejea mapema,” alisema Ally.

Ikumbukwe Simba ndiyo wanashikilia ubingwa huo ambao waliutwaa msimu uliopita kwa kuilaza Yanga mabao 3-1.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic