February 21, 2015


Uongozi wa Stand United umeamua kupora simu za wachezaji wake kuelekea mechi ya Simba.


Stand imefikia uamuzi huo ili kuhakikisha hakuna hujuma kabla ya kuwavaa Simba kesho kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.

Habari za ndani kutoka Stand United zinaeleza kila mchezaji amekabidhi simu yake kwa uongozi.

“Wachezaji wametakiwa kukabidhi simu kwa uongozi na hilo limefanyika kwa ajili ya uhakika tu.

“Si kwamba Simba wametuhujumu, lakini kwa kuwa ni timu kubwa lazima tuwe makini sana katika hili,” kilieleza chanzo.


Stand itakuwa na kazi ya kuizuia Simba kesho ili angalau kukusanya pointi zitakazoikwamua eneo la mkiani.

Tayari Simba iko mjini Shinyanga tayari kwa mechi hiyo inayotarajiwa kuingiza idadi kubwa ya watu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic