April 10, 2015


Mshambuliaji Mkenya wa Simba, Paul Kiongera amesema yuko safi baada ya kurejea uwanjani na kuitumikia KCB ya Kenya ambayo ilimuuza kwa Simba.


Kiongera aliumia goti na kutibiwa nchini India na baada ya hapo Simba ikampeleka kwa mkopo KCB. Tayari uongozi wa Simba ulisema unamrejesha kikosini msimu ujao.

Nyota huyo amekuwa nje akiuguza jeraha la goti alilotonesha akiitumikia Simba katika mchezo wa ufunguzi wa ligi kuu msimu huu dhidi ya Coastal Union, kabla ya Simba kusimamisha mkataba wake kwa muda hadi msimu ujao ambapo ameahidi kurejea Msimbazi.

Akichonga kutoka Nairobi, Kiongera alisema ameshakuwa fiti na kwamba atakuwa uwanjani wiki ijayo kwa mara ya kwanza kuichezea KCB huku akitamba kuwa Kiongera ni yuleyule hata angekaa nje mwaka mzima.


“Namshukuru Mungu, nimepona kabisa na wiki ijayo nina uhakika wa kucheza mchezo wangu wa kwanza katika kikosi changu cha KCB. Nipo hapa kwa mkopo-kulikuwepo makubaliano na Simba kwamba nitakuwa hapa hadi msimu ujao. Tuombe uzima msimu ujao, naweza kuja huko,” alisema.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic