April 10, 2015


Aliyewahi kuwa mdhamini wa Coastal Union, Nassor Binslum, juzi Jumatano alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kulazimika kuondoka uwanjani kabla ya mchezo kumalizika kutokana na kipigo cha mabao 8-0 ilichopokea timu hiyo kutoka kwa Yanga kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.


Binslum ambaye kwa sasa amerejea kuipa sapoti timu hiyo ambayo imeanza kuyumba kwenye ligi, alikuwa uwanjani hapo akishuhudia mchezo huo ambao haukuwa mzuri kwa upande wao.


Binslum ambaye alikuwa amekaa kwenye viti vya jukwaa kuu, aliondoka uwanjani hapo ikiwa ni dakika ya 85 kabla ya mpira kumalizika wakiwa nyuma kwa mabao 6-0, ambapo hakuweza kushuhudia mabao mawili ya Salum Telela na Tambwe yaliyofungwa dakika za 87 na 90.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic