April 9, 2015

 
LUNYAMIKA AKIFAFANUA JAMBO MBELE YA MHARIRI KIONGOZI WA GAZETI LA CHAMPIONI, SALEH ALLY
Tanzania imepangwa katika Kundi G lenye timu za Misri, Nigeria na Chad katika harakati za kuwania kucheza Kombe la Mataifa Afrika mwaka 2017.


Kundi hilo tayari limebandikwa Kundi la Kifo na Watanzania wengi wanaonekana kuingia hofu.

Mmoja wa wachezaji nyota wa zamani wa kikosi cha Tanzania, Taifa Stars, Edibil Lunyamila amesema haoni sababu ya Tanzania kuwa na hofu.

Lunyamila amesema anaamini Watanzania wana kila sababu ya kuamini wanaweza na sasa ndiyo wakati mwafaka wa kuanza maandalizi.

“Sasa ukiihofia Misri, siku nyingine utapangwa na Tunisia au Algeria. Au Ghana na Cameroon, vipi maisha yetu yawe ya woga.

“Kinachotakiwa ni kuanza maandalizi ya uhakika ili kujiandaa,” alisema Lunyamila.
Misri na Nigeria ni kati ya vigogo wa soka la Afrika, hali inayoonekana kuwapa hofu wengi.


Kikosi cha Tanzania chini ya Mholanzi, Mart Nooij kinaonekana kutoaminiwa na wengi kutokana na mwenendo wake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic