April 18, 2015


Habari ya Mbeya kwa sasa ni mechi ya Ligi Kuu Bara inayochezwa leo Jumamosi kwenye Uwanja wa Sokoine kwa kuzikutanisha Mbeya City na Simba.


Tayari mashabiki wengi wameonekana kuwa na pilikapilika za mchezo huo huku kukiwa na kumbukumbu ya Simba kufungwa mabao 2-1 katika mchezo wa mzunguko wa kwanza kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Wakati Simba ikipambana kujihakikishia kufika nafasi ya pili ikiwa na pointi 35 katika nafasi ya tatu, Mbeya City inapambana kuhakikisha haiingii katika hatari ya kushuka daraja kwani ipo nafasi ya kumi ikiwa na pointi 25.

Kocha wa Simba, Mserbia, Goran Koponuvic, akizungumzia mchezo huo, alisema: “Huu ni mchezo mgumu kwangu, tunatakiwa kupambana sana ili tupate ushindi, japokuwa hatutakuwa na Okwi (Emmanuel) kwani mwanzo walitufunga hawa jamaa.”

Kwa upande wa Mbeya City, ofisa habari wa timu hiyo, Dismas Ten, alisema kikosi chao kimeandaliwa vizuri na hakina hofu yoyote dhidi ya Simba.


“Simba ni timu ya kawaida sana na tumejiandaa kama tunavyojiandaa kucheza na timu nyingine za ligi kuu, tunahitaji pointi tatu na wachezaji wote wako fiti kwa ajili ya mchezo huu,” alisema Ten.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic