April 18, 2015


Kocha wa Yanga, Hans van Der Pluijm ametazama video za mechi za Etoile du Sahel na kusema amegundua kikosi chao kina tatizo la mabeki wanaocheza taratibu mno.


Kutokana na kugundua udhaifu huo wa safu ya ulinzi ya Waarabu hao wa Tunisia, Pluijm amepanga kuwatumia kwa pamoja mawinga wenye kasi Simon Msuva na Mrisho Ngassa kuwachosha mapema wapinzani wao.

Katika mazoezi ya jana asubuhi kwenye Uwanja wa Karume, Pluijm alionekana akitumia muda mwingi kuwaelekeza Msuva na Ngassa jinsi ya kuiwahi mipira mirefu itakayokuwa ikipelekwa kwao na viungo.

“Inabidi tucheze kwa kasi sana, kwani mabeki wa Etoile hawana kasi lakini washambuliaji wao wana kasi hivyo ni wazuri wakiwa na mpira, sasa tutatumia udhaifu wao nyuma lakini lazima tujilinde kwa washambuliaji wao,” alisema Pluijm raia wa Uholanzi.


Akizungumzia mchezo huo, Msuva alisema: “Nimejipanga kufanya vizuri dhidi ya Etoile kwani kocha amenielekeza kuhusu nini cha kufanya na natakiwa kukimbia sana katika kushambulia.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic