August 9, 2015

Unamkumbuka yuko kiungo mchezeshaji wa zamani wa Mtibwa Sugar na Yanga, Abdi Kassim ‘Babi’, bado anaendelea kung’ara nchini Malaysia.

Wikiendi hii ameingoza timu yake ya UiTM FC kuichapa Sabah FC kwamabao 3-1.

Babi akiwa nahodha, El Hadji Diouf raia wa Senegal akiwa nahodha wa Sabah FC, bado hakuweza kuzuia makali ya kikosi cha Mtanzania huyo.

Diouf ni mmoja wa wachezaji nyota barani Afrika na amewahi kung'ara akiwa na Liverpool na Bolton akikipiga nchini England.

Akizungumza kutoka Al Shah Alam, Malaysia Babi amesema wamekuwa na mwendno mzuri ingawa si sana.

“Ligi ni ngumu na tunaendelea kupambana, baada ya ushindi huo dhidi ya kina Diouf tumesogea hadi nafasi ya nane sasa,” alisema.


Tayari Babi ameishatupia mabao nane nyavuni na ndiyo kiungo tegemeo wa UiTM FC.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic