October 22, 2015



Juhudi za Kamati ya timu ya soka ya taifa, Taifa Stars bado zinaendelea kuhakikisha inapatikana sehemu sahihi kwa ajili ya kambi kujiandaa kuing’oa Algeria kuwania kucheza Kombe la Dunia.
Kamati hiyo imesema kuwa kuna sehemu tatu ambazo zinafanyiwa kazi kabla ya kupata moja ambayo itakuwa sahihi.
Zimetajwa kuwa ni Afrika Kusini na itakuwa katika mji tulivu wa Pretoria, Oman katika jiji la Muscat au Dubai ndani ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).
Katibu na msemaji wa Kamati ya Taifa Stars, Teddy Mapunda alisema bado mazungumzo na vyama vya soka nchi hizo yanaendelea na mambo yakikaa sawa, watatangaza ni nchi gani kikosi kitaenda kuweka kambi.
“Bado mazungumzo na FA za nchi ambazo tumeaona ni pa zuri pa kuweka kambi yanaendelea, hivyo mambo yakikaa sawa, muda wowote tutawatangazia ni wapi kikosi chetu kitaweka kambi yake,” alisema Mapunda.
Kwa upande mwingine, aliwaomba Watanzania kuisapoti kamati yao yenye jukumu la kuhakikisha Algeria inachapwa pamoja na ukubwa wa jina lake kwenye soka barani Afrika, ikiwa kileleni kwa ubora.
“Tunaomba Watanzania kutupa mchango wa Sh 100 ambazo zinakwenda kufanya mambo mbalimbali kama kuboresha kambi ya kikosi, motisha kwa wachezaji, chakula na mambo mengine kama sehemu ya kuandaa mazingira mazuri ya timu,” aliongeza Teddy.
Kiasi hicho kitumwe katika namba: 0654 888 868 au 0789 530 668.
Kamati hiyo ipo bado inaendelea na mazungumzo kwa ajili ya kupata ndege ya kukodi kwa ajili ya Watanzania watakaotaka kwenda kuisapoti Stars katika mchezo wa marudiano huku Algeria. Nauli itatangazwa baadaye.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic