October 24, 2015


Kocha Abdallah Kibadeni ameanza kwa mkwara kazi ya kuinoa JKT Ruvu kwa kufumua kikosi cha kwanza ambapo mabadiliko hayo yaliiwezesha timu hiyo kutoka suluhu na Mtibwa Sugar juzi Alhamisi.

Katika mchezo huo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam, Kibadeni alikuwa anaiongoza timu hiyo kwa mara ya kwanza huku akiwa amefanya mabadiliko kadhaa.

Kibadeni amemtumia Shaaban Dihile kwa mara ya kwanza kikosini akichukua nafasi ya Hamis Seif, pia kiungo Issa Ngao naye amejumuishwa kikosini kwa sasa.

Kocha huyo aliyewahi kucheza na kuifundisha Simba, amesema huwa anawatumia wachezaji waliofanya vizuri mazoezini siku tatu kabla ya mechi.

“Hiki kikosi unachokiona kilichocheza leo (juzi) dhidi ya Mtibwa, karibu chote nimekifanyia mabadiliko, baadhi wanacheza kwa mara ya kwanza na wengine nimewabadilisha nafasi ili tupate ushindi,” alisema.


Licha ya matokeo hayo, bado JKT Ruvu ipo mkiani mwa ligi kuu ikiwa na pointi mbili tu katika mechi saba ilizocheza hadi sasa. Kibadeni amechukua nafasi ya Fred Minziro aliyejiuzulu kutokana na matokeo mabovu ya timu hiyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic