November 13, 2015

HASSANOO AKIWA MAHAKAMANI KISUTU. HII ILIKUWA NI MIEZI KADHAA ILIYOPITA ALIPOKATALIWA DHAMANA.
Katibu Mkuu wa zamani wa Simba, Hassan Othman 'Hasanoo' ameachiwa kwa dhamana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kukaa mahabusu kwa muda wa miaka mitatu.

Hasanoo aliwekwa ndani akikabiliwa na mashtaka matatu likiwemo kosa la kuhujumu uchumi  na kusafirisha pembe za ndovu zenye thamani ya Sh bilioni 1.1 kwenda Hong Kong, China.

Mbali na kesi hiyo pia anakabiliwa na kesi ya wizi wa tani 26.475 za madini ya Shaba zenye thamani ya Sh 333, 467,848.13 kutoka Zambia kinyume na kifungu cha sheria namba 258, 265 na 269 (C) vya kanuni ya adhabu mali ya Kampuni ya Liberty Express Tanzania Ltd ambayo ilifunguliwa mahakamani hapo na mwendesha mashtaka wa serikali DPP.

Mahakama hiyo ilikubali kumuachia kwa dhamana baada wadhamini wa Hasanoo kukidhi vigezo vya dhamana vilivyowekwa.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic