September 28, 2017


Gumzo la mechi ya watani Yanga na Simba itakayochezwa Oktoba 28 limezidi kupanda baada ya kuelezwa kuwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, utakuwa katika matengenezo.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe alisema jana, uwanja huo unahitaji muda wa miezi mitatu zaidi na akaahidi utakuwa bomba ile mbaya.

Tayari kampuni ya kubashiri ya SportPesa imeanza kufanya ukarabati katika uwanja huo.

Lakini taarifa hiyo, kwamba hadi Oktoba 28 uwanja utakuwa katika matengenezo inaonekana kuwashitua mashabiki wengi.


Tayari kumezuka mijadala kuhusiana na wapi watani hao watacheza mechi yao hiyo.

Mashabiki wengi wangependa kuona timu hizo zinacheza kwenye uwanja huo kama ilivyozoeleka.

Wengi wamekuwa wakihoji kama Uwanja wa Uhuru unaweza kuibeba mechi hiyo ana wengine wameshauri mechi ihamishiwe CCM Kirumba, Mwanza.

Lakini wako wanatania kuwa hata Chamazi itatosha na wamekuwa wakishambuliwa kuwa hawako makini katika jambo muhimu.

Bado halijawa tamko rasmi au Yanga na Simba hazijapata barua baada ya maneno ya waziri, huenda zikajadiliana na kutangaza wapi zingependa kwenda.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic