May 8, 2019


MSHAMBULIAJI wa timu ya Simba ya Dar es Salaam, John Bocco, amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa mwezi Aprili wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) msimu wa 2018/2019. 

Bocco ametwaa tuzo hiyo baada ya kuwashinda wenzake wawili, Emmanuel Okwi wa Simba na Heritier Makambo wa Yanga alioingia nao fainali katika uchambuzi uliofanywa Dar es Salaam wiki hii na Kamati ya Tuzo ya TPL inayotolewa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). 

Kwa mwezi huo wa Aprili, Simba ilicheza michezo sita na kushinda mitano na kupoteza mmoja, ambapo Bocco alitoa mchango mkubwa kwa timu yake akifunga mabao matatu na kuifanya Simba ipande hadi nafasi ya pili ikitoka ya tatu iliyokuwepo mwezi uliopita.

Kwa upande wa Makambo yeye aliiongoza Yanga iliyocheza michezo mitano ikishinda mitatu, sare mmoja na kupoteza mmoja, ambapo alifunga mabao matatu na alikuwa na mchango mkubwa katika mafanikio ya Yanga kuendelea kubaki nafasi ya kwanza mwezi huo, wakati Okwi aliyefunga pia mabao matatu alikuwa chachu ya mafanikio ya Simba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic