July 13, 2019



ELIAS Maguli huenda akatua nchini Kenya kusakata soka la kulipwa iwapo atakubali masharti ya mabosi wa timu mpya inayoshiriki Ligi Kuu ya Kenya msimu ujao.

Imeelezwa kuwa Maguli ambaye ni mshambuliaji huru baada ya kuachana na timu yake ya KMC ameingia kwenye anga za timu ya Gor Mahia ambayo inaendelea kusuka kikosi chake.

“Kama ambavyo wameanza na mchezaji kutoka Singida United, David Kissu sasa mpango uliopo ni kumpata mshambuliaji ambaye hatakuwa wa gharama kubwa zaidi kwani mambo mengi hayajawa sawa, na anayetajwa ni Maguli,” kilieleza chanzo hicho.

Maguli amesema kuwa mchezaji kazi yake kubwa ni kucheza hivyo hana tatizo na uwezo wake ni suala la muda tu kujua hatma yake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic