July 13, 2019



WACHEZAJI wengi kwa sasa wanachekelea kusaini kandarasi ya miaka mitatu ama miwili kwenye vikosi vipya hili ni jambo jema lakini je wanaangalia mbele ama macho kwenye noti?

Naona kila mmoja anafurahi kuanza changamoto mpya mwisho wa siku anapotea na kusahaulika kabisa kwenye ramani ya mpira.

Wachezaji wanapaswa wawe na maamuzi magumu na sahihi ifike wakati watazame namna bora itakayokuza viwango vyao kwanza kabla ya kukimbilia pesa ambazo zinawafanya wafurahi kwa muda.

Furaha ya mchezaji ambayo anaipata kwa kujiunga na timu itakayompa fedha huwa ni ya muda mfupi baada ya msimu kuisha ndoto zake zinayeyuka kabisa.

Ukweli ni kwamba wakati huu wa usajili ni muhimu kwa wachezji kujiuliza mara mbili wanakwenda kucheza timu gani na wanagombania namba na nani?

Endapo atajiuliza maswali haya itakuwa rahisi kwake kutoa maamuzi sahihi yatakayomfanya aamue kusaini ama kubaki kwenye timu yake ambayo anaitumikia kwa sasa.

Kama mchezaji atafurahia dau alilowekewa mezani ilihali hana nafasi ya kucheza ni bora aachane na hilo dili kwani litakuja kumgharimu baadaye.

Kama atakomaa ili ajiunge na timu ambayo ina wachezaji wa kutosha gharama ya furaha ya muda atailipa baadaye atakapokuwa anasugua benchi na kukumbuka kule alikotoka.

Muda wa furaha kwa wachezaji ambao wana uwezo wa kawaida huwa wa muda lakini muda wa majuto huwa ni mkubwa na wa kudumu.

Nina mifano ya wachezaji wengi ambao ni marafiki zangu pia awali walikuwa wanafurahia kusaini kwenye timu walizozipenda mwisho wa siku wakapoteza furaha yao kwa kukosa namba.

Wapo ambao walikumbuka namna walivyokuwa wanapata nafasi kwenye timu zao za zamani ila mwisho wa siku wakawa wameshapoteza dira.

Ukiachana na hao wapo wale ambao walikuwa na rekodi nzuri walipotoka timu zao za awali ila walipojiunga na timu nyingine walipoteana kabisa.

Ni wakati wa wachezaji kutazama timu anayokwenda kucheza na kuangalia nafasi yake kama ataona itakuwa ngumu kushindani ni kheri aache kwanza.

Siku zote riziki ni kama ajali huja bila taarifa endapo mchezaji ataamua kulazimisha mambo matokeo yake yatakuwa yenye maumivu kwake.

Itakuwa busara kwa wachezaji kufanya uchunguzi mdogo kabla ya kukubali kujiunga na timu ambayo imempa dili mezani asikimbilie kusaini.

Majuto siku zote ni mjukuu kabla ya kufika muda wa majuto wakati huu uliopo ni sahihi kwa mchezaji kusoma alama za nyakati kabla ya kukimbilia kujifunga na timu yake mpya.

Wapo wachezaji ambao sajili zao zilitikisa mwisho wa siku wakaishia kusugua benchi na kukimbia timu kwa kukosa kile ambacho walikuwa wakikipata.

Wengine walitolewa kwa mkopo ili kukuza viwango vyao na mwisho wa siku wakawa wameshapoteza ujasiri wa kurejea kwenye ubora wao wakabaki kuwa wachezaji wa kawaida ambao soko likawakataa mara ya pili.

1 COMMENTS:

  1. Tatizo lipo hapa kwa vijana wetu wengi wa kitanzania ni kuendeleza furaha nakuwa starehe ndani ya kazi baada ya kubahatika kupata mkataba wenye maslahi mazuri na hicho ndicho kitu kinachowamaliza.vijana wetu wengi hawana eleimu ya kazi yao na miiko yake.Mpira kazi inayotegemea uwezo wa kujituma wa mtu binafsi kwanza na team work inafuta baadae.Mchezaji hawezi kubweteka kwakuwa tu amesajiliwa kwenye timu yenye wachezaji wazuri na yeye atakuwa mzuri hapana. Kwa mchezaji wa mpira mwenye malengo makubwa zaidi hasa vijana Tanzania bado hapajafikia kiwango cha kumfanya mchezaji abweteke na hela ya mkataba.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic