BEKI wa klabu ya Valencia, Alessandro Florenzi ametengwa kwa
miezi miwili sasa baada ya kukutwa na maambukizi ya aina tofauti.
Beki huyo awali alitengwa peke
yake kwa mwezi mmoja baada ya kuugua tetekuwanga(Chikenpox) lakini sasa ametengwa
kwa mwezi mmoja baada ya kupata maambukizi ya Virusi vya Corona.
Mchezaji huyo alijiunga na
Valencia kwa mkopo Januari mwaka huu akitokea katika klabu ya Roma.
Hivi karibuni
alipimwa Virusi vya Corona na akakutwa na virusi lakini
alipojipima mwenyewe majibu yameonyesha kuwa hana maambukizi.
Florenzi baada ya kutengwa awali
alikosa mechi dhidi ya Atletico Madrid, Atalanata na Real Sociedad, lakini
baadaye alicheza dhidi ya Real Betis na alikaa benchi mechi dhidi ya Alaves na
Atalanta.
Beki huyo kwa msimu huu amecheza
dakika 160 tu kabla ya La Liga kupigwa stop kutokana na mlipuko wa Virusi vya
Corona.
0 COMMENTS:
Post a Comment