May 6, 2020



KLABU ya Simba, leo Mei 6, 2020, imeazimisha miaka nane tangu ilipowanyuka watani zao wa jadi Yanga mabao 5-0.

Simba katika msimu wa 2011/12, iliifunga Yanga mabao 5-0 katika mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu Bara msimu huo na kutwaa ubingwa chini ya Kocha, Milovan Cirkovic raia wa Serbia.

Katika mchezo huo uliochezwa Mei 6, 2012 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, mabao ya Simba yalifungwa na Emmanuel Okwi dakika ya kwanza na 62, Felix Sunzu (dk 53), Juma Kaseja (dk 66) na marehemu Patrick Mafisango (dk 71).

Kupitia mitandao yao ya kijamii, Klabu ya Simba leo imeposti taarifa hiyo na kuandika: “Tarehe nzuri kwa Wanasimba, mbaya kwa mashabiki wa mtani. Historia muhimu (tarehe kama ya leo mwaka 2012).”

6 COMMENTS:

  1. Hebu tusisahau zile tarehe Simba alipopigwa 5/5 na Al ahli na motema pembe

    ReplyDelete
    Replies
    1. Pia tusisahau Yanga tarehe kama hizo Yanga alipigwa 6-0 na Raja casablanca

      Delete
  2. Ha ha ha ha ha ha ha kiroho kinakuuma brother,na wewe siutaikumbuka tarehe mliyoifunga simba goli moja kupitia kwa morison,mpaka mnashawishi ligi ifutwe mlivyokua na akili finyu,yanga mna shida sana na kwakuwashauri punguzeni mihemko ndugu zangu maisha hayataki pupa mtajikuta mnapoteza kila kitu kwa ujinga wenu.

    ReplyDelete
  3. Yaliyopita si ndwele tugange yajayo yanafurahisha......yanga mpango mzimaaa utaipenda hata kwakuforce

    ReplyDelete
  4. Mei 1/1968 yanga ilifanya nini kwa Simba 5-0 Kwahyo Hayo ni matokeo ya uwanjani

    ReplyDelete
  5. Daaa hata Leo 25/9/2021 ngao ya jamii mbona hakuna mashabiki kunanani jamanii

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic