April 27, 2021


HAKUNA maisha mazuri kama yale ya kupanga kushinda kisha ukafeli kushinda kile ulichokipanga hapo nina amini kwamba kuna jambo ambalo utakuwa umejifunza.

Ni ngumu kuamini kwamba kwenye ulimwengu wa soka zile timu ambazo zilishuka daraja nguvu zao Ligi Daraja la Kwanza huwa inakuwa ndogo na mwisho wa siku zinaangukia Ligi Daraja la Pili, kisha baadaye zinaanza upya kwenye Ligi ya Mkoa.

Awali ilikuwa ni ndoto mbaya kuota kwamba Singida United itashuka daraja na itashiriki Ligi Daraja la Kwanza kisha huko itakwama na kushushwa tena kutokana na makosa ambayo wanaweza kuyafanya.

Ila imekuwa hivyo sasa wao maisha yao Ligi Kuu Bara yaliwashinda, kisha wakaangukia Ligi Daraja la Kwanza huko nako wakashindwa na kushushwa kutokana na kushishindwa kupeleka timu uwanjani, ajabu na kweli.

Bado sijajua timu ambazo huwa zinapanda kwa kasi na kufanya vizuri huwa zinakumbwa na nini hasa zinapoanza kushiriki Ligi Kuu Bara.

Ninavuta picha ile Mbeya City yenyewe ambayo ilikuwa inaishi kwenye dunia yake ya ushindani namna ambavyo ilikuwa inaingia uwanjani kupambana na vigogo kama Simba na Yanga.

Ile Mbeya City ambayo shabiki wa Dar alikuwa anakubali kuvua uzi wa njano na ule mwekundu ama ule mweusi na mweupe kisha anavaa ule wa Mbeya City.

Leo hii mbeya City inapambana na hali yake ndani ya Ligi Kuu Bara huku ikiwa haina uhakika wa msimu ujao kushiriki tena kwenye ligi hii labda inaweza kuangukia Ligi Daraja la Kwanza.

Unaikumbuka ile Mtibwa Sugar yenyewe ambayo ilikuwa ikiingia Uwanja wa Mkapa hata Uhuru mpinzani anaanza kujiuliza mara mbilimbili namna gani anaweza kupata ushindi?

Nguvu ilizimika ghafla baada ya timu hiyo kutwaa taji la Mapinduzi, Visiwani Zanzibar. Iliporudi kwenye ligi mambo yakawa tofauti.

Uongozi wa Mtibwa Sugar uliweka wazi kwamba mkwanja ambao walipewa wachezaji wao baada ya ushindi huo uliwapumbaza na kuwafanya wasahau kuongeza juhudi, ajabu nyingine.

Leo hii ikiwa inapambana kutetea nafasi yake kubaki ndani ya ligi unaambiwa kwamba kumbe Dickson Job alikuwa mhimili kwa kuwa ameondoka kaondoka na nguvu ya ushindi.

Inawezekanaje sasa timu bora na imara kama Mtibwa Sugar kuyumbishwa na beki? Sawa inawezekana kwa kuwa alikuwa nahodha ila je wakati wanafanya biashara hawakatambua kwamba ni lazima atafutwe mbadala wake.

Asanteni sana Mtibwa Sugar kwa kuonyesha ukomavu wenu na kuendelea kupambana, bado nina amini mashabiki wenu wanawaombea dua ili mbaki kila la kheri.

Ukirudi kwa Ndanda FC hawa nao safari yao ya kushuka kutoka Ligi Kuu Bara ilikuwa ni kutokana na ukata na sasa ndani ya Ligi Daraja la Kwanza mambo yamegoma tena sababu ileile ya ukata.

Hapa hili tatizo inabidi litafutiwe ufumbuzi na wamiliki wa timu pamoja na Shirikisho la Soka Tanzania, (TFF) kuangalia namna ya kuzipa sapoti timu hizi.

Itazame Njombe Mji, ilikuwa inarejea taratibu wakati ligi ilipoanza msimu huu na matumaini yalikuwa makubwa, ghafla nayo inapambana kubaki ndani ya Ligi Daraja la Kwanza.

Sijui itakuaje ikiwa itashuka Ligi Daraja la Kwanza, mambo yatakuwa magumu kwa kuwa unaambiwa lile lijalo ni gumu kuliko lile ambalo linaisha kwa wakati huu.

Wana Lipuli bado hapo Kamwene kama haijaeleweka hivi ni muhimu kupiga hesabu upya na kuona namna gani timu za nyanda ya Kusini zinaweza kuwa na nguvu kwenye Ligi Kuu Bara.

Kwa hali ilivyo ikiwa Njombe Mji haitazinduka kwa sasa naiona kule Ligi Daraja la Pili itaungana na Boma FC ya Mbeya, Ndanda FC ya Mtwara ambazo hizi zimeweka wazi kwamba hazina nafasi ya kubaki kwenye Ligi Daraja la Kwanza.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic