August 22, 2021

UONGOZI wa klabu ya Yanga umeweka wazi kuwa upo katika mazungumzo ya kuwaongeza mikataba kocha msaidi wa timu hiyo, kocha wa viungo na daktari wa misuli mara baada ya mikataba yao ya awali kutamatika ndani ya Yanga.

Kocha Msaidizi, Sghir Hammadi mwenye uraia wa Tunisia, kocha wa viungo Mmorocco, Jawab Sabri na Mchua misuli wa Yanga  mwenye uraia wa Afrika Kusini, Fareed Cassiem wote hawapo katika kambi ya Yanga iliyopo nchini Morocco.

Yanga kwa sasa ipo nchini Morocco ambapo klabu hiyo imeweka kambi maalumu ya siku 10 kwa ajili ya  maandalizi ya msimu mpya, wa michuano mbalimbali ambayo Yanga itashiriki katika msimu ujao.

Chanzo cha ndani kutoka Yanga kimetuambia kuwa makocha hao wote watatu wamemaliza mikataba yao, huku wengine wakiwa wapo katika mazungumzo na timu nyingine japo klabu ya Yanga wapo katika mazungumzo ya kuwaongezea mikataba mipya.

“Ni kweli makocha hao wote mikataba yao imetamatika ndani ya Yanga, na wapo ambao walikuwa kwenye mazungumzo ya kujiunga na klabu zingine huku Yanga nao wakifanya nao mazungumzo ya kuhitaji kuwaongezea mikataba mipya.

Akizungumzia sakata hilo Ofisa habari wa Yanga Hassani Bumbuli amesema: “Mikataba ya makocha hao imemalizika hivyo kama klabu tupo katika mipango ya kuwaongezea mikataba mipya hivyo wanaweza wakaonekana msimu ujao, au wasionekane,” Amesema kiongozi huyo.


9 COMMENTS:

  1. Ingekuwa Simba vingetengenezwa vipindi maalum kwanini wasiwaongezee mikataba kabla. Kwa Utopolo kimyaa. Hizi njama za wachambuzi uchwara hazitawafikisha popote.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Sijui mnawaza kwa kupitia makalio mashabiki wa mikia? Umewahi kuona kipindi Maalum cha kuzungumzia makocha wasaidizi wa timu yenu?

      Delete
  2. Waandishi uchwara wote kimyaaa. Wako bize kuokoteza uzushi kuhusu simba. Andikeni hayo sasa

    ReplyDelete
  3. Hahahaha upuuzi na ushuzi tu ndo umeandikwa hapo, et chanzo cha kuaminika! Nyie mko hapa bongo timu iko morroco arafu hata chanzo hujaweka unasema et chanzo cha kuaminika! Nguruwe fc wewe

    ReplyDelete
  4. Kwahiyo hata hapo gazeti la salehjembe mtu akimaliza mkataba wake wa kazi unataka uandike stori ya kuleta mjadala? Mbona ni kitu cha kawaida ambacho hakihitaji mjadala

    ReplyDelete
  5. Nini yanga faida waliopata kutokana na kambi yao Morocco. Mimi nahisi walikwenda kutembea na kurudi nyumbani na kulalamika joto kali wakimuacha Myama aendelee na kile na kile walichokudia nacho. Kwanza waliisifu hali ya hewa na kusema ni kama ile ya nhumbani. Si bure

    ReplyDelete
  6. Kichwa Cha habar na maelezo haviendani kabisaa so wandish mnazingua Sana na maelezo yenu.

    ReplyDelete
  7. Nikishaona mwandishi ni salehe jembe si a haha ya kusoma kilichoandikwa na jua ni pumba tupu

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic