Geilson Santana ‘Jaja’ ameamka baada ya
kuifungia Yanga bao lake la kwanza kwenye Ligi Kuu Bara kwenye ushindi wa mabao
3-0 dhidi ya Stand United.
Lakini Jerry Tegete ndiye alikuwa kivutio
baada ya kuingia kipindi cha pili na kupachika mabao mawili peke yake.
Tegete aliyeingia dakika ya 70 kuchukua
nafasi ya Jaja, alifunga bao lake la kwanza katika dakika ya 77, likiwa la pili
kwa Yanga, kabla ya kufunga la pili katika dakika ya 90.
Jaja alifunga bao lake mapema tu katika
dakika ya 12 baada ya mpira kumkuta akiwa katika nafasi nzuri na kupiga fasta
ukajaa wavuni.
Mechi hiyo kwenye Uwanja wa Kambarage
ilikuwa nzuri huku Stand wakionyesha soka safi.
Hata hivyo Stand walikuwa na tatizo la
umaliziaji kwani walishindwa kufunga kila walipoingia kwenye lango la Yanga.
Kuingia kwa Tegete na Hussein Javu
kuliongeza kasi zaidi.
0 COMMENTS:
Post a Comment