MPIRA UMEKWISHA:
MWAMUZI SIMON MBERWA ANAPULIZA FILIMBI YA MWISHO KATIKA DAKIKA 90.
Dk 90+3
MWAMUZI SIMON MBERWA ANAPULIZA FILIMBI YA MWISHO KATIKA DAKIKA 90.
Dk 90+3
Dk 87 Ally Nassor anapiga shuti kali lakini
linapaa juu ya lango la Yanga
GOOOOOO Dk 83, Tambwe anaifungia Yanga bonge
la bao kwa kichwa baada ya krosi ya Msuva
Dk 82, Msuva anapiga kichwa tena lakini
kinakuwa lakini kwa kipa wa Mgambo.
Dk 78, anatolewa Sherman anaingia Hussein
Javu
GOOOOOOOO Dk 77, Msuva anaifungia Yanga bao baada ya purukushani katika lango la Mgambo.Dk 75, krosi safi ya Joshua, mpira unatua kichwani mwa Tambwe lakini kipa wake anakuwa fundi na kudaka.
Dk 69, shuti kali la Niyonzima linaokolewa na kipa wa Mgambo na kuwa kona isiyo na matunda.
Dk 67, Yanga wanafanya mashambulizi
mfululizo lakini Mgambo wanaokoa tena.
Dk 66 krosi nzuri ya Niyonzima, mabeki
Mgambo wanaokoa na kuwa kona.
Dk 60 Msuva anaiwahi vizuri krosi ya Juma
Abdul na kupiga vizuri lakini inagonga mwamba na kutoka nje.Dk 53, Sherman anajaribu shuti kali lakini linapaa juu.
Dk 50, Msuva analambwa kadi ya njano
kutokana na kucheza faulo ya makusudi. Halikadhalika Salim Mlima wa Mgambo naye anapigwa kadi ya njano.
Dk 47, Fullyzully Maganga analambwa kadi ya
njano kwa kujiangusha.
Dk 46 Tambwe anapiga shuti linagonga mwamba.
MAPUMZIKO:Dk 45 Msuva anapata pasi nyingine safi kutoka kwa Niyonzima. Lakini anapiga shuti ‘mtoto’
Dk 42, Msuva anapata nafasi nyingine nzuri baada ya pasi ya Sherman lakini anashindwa kufunga. Kocha Hans anasimama na kuanza kufoka.
Dk 40, Said Juma Makapu analambwa kadi ya njano kwa faulo mbaya.
Dk 32, Msuva anapata nafasi nzuri lakini
akiwa amebaki na kipa anabutua juuu.
Mechi imeanza kwa kasi licha ya uwanja kuwa
umeloa tope.
Yanga ndiyo wanaonekana kuwa vizuri zaidi
kutokana na kupeleka mashambulizi mengi zaidi.
Iwapo Yanga watatulia, basi wanawza kupata
bao.
0 COMMENTS:
Post a Comment