Mvua inayoendelea kunyesha mjini Tanga inaonyesha kumpa hofu Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm.
Pluijm amesema anaingia hofu kabla ya kuivaa Mgambo Shooting kwenye Uwanja wa Mkwakwani leo kwa kuwa uwanja utakuwa kikwazo.
"Jana tulilazimika kusitisha mazoezi kutokana na mvua. Sasa leo imenyesha usiku wote na inaendelea. Kidogo inanitisha.
"Lakini sisi ni timu, tutalifanyia kazi suala hilo na kujua nini cha kufanya," alisema.
Jana, Yanga ilifanya mazoezi kwa dakika 40 kabla ya kusitisha kutokana na mvua kubwa kunyesha wakiwa mazoezi kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.
0 COMMENTS:
Post a Comment