March 21, 2015


Mvua inayoendelea kunyesha mjini Tanga inaonyesha kumpa hofu Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm.
Yanga inashuka dimbani leo kuwavaa Mgambo Shooting kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.

Pluijm amesema anaingia hofu kabla ya kuivaa Mgambo Shooting kwenye Uwanja wa Mkwakwani leo kwa kuwa uwanja utakuwa kikwazo.

"Jana tulilazimika kusitisha mazoezi kutokana na mvua. Sasa leo imenyesha usiku wote na inaendelea. Kidogo inanitisha.

"Lakini sisi ni timu, tutalifanyia kazi suala hilo na kujua nini cha kufanya," alisema.

Jana, Yanga ilifanya mazoezi kwa dakika 40 kabla ya kusitisha kutokana na mvua kubwa kunyesha wakiwa mazoezi kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.






0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic