AKISIMAMA mtu akasema Watanzania ni waoga
kupindukia, utaona watu watakavyopandwa jazba kama vile wametukanwa tusi kubwa
sana au kudhalilishwa.
Hao watakaopinga au kukasirishwa, wanajua
ukweli kwamba Watanzania ni waoga hata kwenye mambo ya kawaida sana. Sisemi
waingie kwenye fujo au vurugu ambalo ni jambo baya sana, nazungumzia angalau
kwenye kupasa sauti na kutete hoja zao za msingi.
Acha mimi nionekane mkorofi linapofikia
suala la kutetea nchi kwa kuwa wengi wetu tunajisahau na kuwatukuza Wazungu
tukiamini wanajua kila jambo, kitu ambacho si sahihi hata kidogo.
Kocha wa Taifa Stars, Mart Nooij ametangaza
kikosi kitakachocheza mechi ya kirafiki dhidi ya Malawi kwenye Uwanja wa CCM
Kirumba mjini Mwanza.
Kocha huyo raia wa Uholanzi ameita kikosi
chake kilekile bila ya kuangalia vigezo ambavyo wote tunavijua. Haihitaji kuwa
kocha kutoka Ulaya ili kuelewa uteuzi wa kikosi.
Nooij amemuacha kipa Ally Mustafa ‘Barthez’
na kuwachukua Mwadini Ally, Aishi Manula pamoja na Deogratius Munish ‘Dida’
ambaye amekuwa benchi kwa zaidi ya mechi saba.
Amewachukua mabeki wawili wakongwe wa
pembeni, Oscar Joshua (Yanga) na Erasto Nyoni (Azam FC), sawa! Lakini
hakuangalia kuwa kuna mabeki makinda ambao wanafanya vizuri zaidi.
Mabeki wawili wa Simba, Mohammed Hussein
‘Tshabalala’, Hassan Kessy na David Luhende (Mtibwa Sugar) angalau wawili kati
yao.
Kuna viungo wangapi wangecheza badala ya
mkongwe Amri Kiemba ambaye anaweza kutangaza kustaafu hivi karibuni?
Kwa washambuliaji, kumchukua John Bocco
wakati akijua kuna wengine wanaofanya vizuri kama Rashid Mandawa (Kagera Sugar)
au Samuel Kamuntu (JKT)? Wakati anamchagua, Bocco alikuwa na mabao moja, sasa
ana mawili! Kamuntu ana saba na Mandawa nane.
Lakini vipi Ibrahim Ajib, Abdi Banda, Jonas
Mkude na Said Juma ‘Makapu’ ambao wameonyesha kuwa na uwezo kweli?
Asingeweza kuwaita wote hao niliowataja,
lakini angalau nusu yao na kocha mwenye hesabu na kikosi chake basi huangalia
kutumia vijana hasa katika kipindi ambacho hakina mashindano.
Kwa alichofanya Nooij anaonyesha wazi hana
mipango ya muda mrefu na Stars. Ndiyo maana anachoangalia ni rekodi zake,
hataki kufungwa na anahitaji wachezaji wakongwe wampe matokeo.
Anataka rekodi zake ziwe safi zaidi hata
baada ya kuondoka Stars, apate timu kwingine. Haangalii Tanzania itaathiika
vipi kwa kuwa wachezaji wake wanazidi kuzeeka na hakuna waliopata nafasi ya
kuwaridhi.
Kiemba atakayestaafu baada ya miaka
michache, si bora angeitwa Ajibu ambaye ataendelea kucheza kwa miaka mingine
nane au zaidi? Nani anaweza kusema Mholanzi huyo hajui hilo.
Anaamua kuwaita hadi makipa wanaokaa benchi
na kuacha wanaodaka. Najiuliza anapoonekana kwenye Uwanja wa Taifa au Chamazi
Complex amekuwa akienda kufanya nini hasa kama anakuwa na kikosi chake
kichwani.
Bado siamini Zanzibar hawana wachezaji
mahiri au bora wanaoweza kupata nafasi katika kikosi cha Stars. Tuliona
michuano ya Mapinduzi ilivyokuwa migumu na wachezaji kadhaa walizisumbua timu
za Bara. Wako wapi waliofanya vema Mapinduzi?
Kipindi chote hiki kazi kubwa ya kocha huyo
huwa ni nini hasa? Kuchukua tu mshahara TFF? Maana kikosi chake anacho
kichwani, sasa nini hasa anachofanya na kuisaidia nchi yetu?
Najua kwa uoga wenu wengi, mtaona kocha
kaonewa. Lakini lazima kuwekwe utaratibu wa kuwabana makocha wanaofanya mambo
kwa kuripua huku wakichota fedha za Watanzania.
Lazima wapewe changamoto na wajue wanafanya
kazi na watu wanaoelewa mambo. Hivyo si wafanye wanachotaka kwa kuwa wanajua
wanatoka Ulaya.
Tanzania ni zaidi ya Ulaya, tunakosa vichache, si wakija hapa,
wazidi kutokosesha badala ya kutusaidia. Akiendelea hivyo, basi kamwe sitakaa
kimya, Tanzania si sehemu ya piknik.
Tatizo ni TFF, wakati wanamchukua waliangalia CV yake na kuielewa!! Kuna makocha ni wa matokeo kama ilivyo kwa Mou, Benetez nk lakini wapo makocha wa kuendeleza vipaji kama Arsene w., Ancellot nk. Lakinibpia kocha kabla ya kumpa mkataba unatakiwa umpe malengo yako na yeye akupe program ya ku-achieve hayo malengo ndo muingie mkataba!! Kama haukufanya hivyo unamu-assess vipi mwalim maana hakuna TOR
ReplyDelete