Wachezaji wa Yanga
wametakiwa kujituma zaidi kwa kuwa mambo bado hayajakaa kama anavyotaka kocha
wao Hans van der Pluijm.
Pluijm raia wa Uholanzi
amesema anaamini wachezaji wa Yanga wanaweza kufanya vizuri zaidi ya
wanavyofanya sasa.
“Lakini haiwezi kuwa lahisi
kama watajisahau. Hivyo nimekuwa nikiwasisitiza kujituma kila mara.
“Mafanikio yakipatikana
wengi hujisahau mapema, mimi naona wachezaji wanaweza kufanya vizuri zaidi ya
hapa.
“Kikosi changu ni bora
lakini bado naamini kina ubora zaidi. Hatuwezi kufanikiwa bila ya kujituma.
“Najua kujifunza ni kufanya
mambo tena, tena na tena bila ya kuchoka na ndiyo tumekuwa tukiendelea kufanya
hivyo,” alisema Pluijm.
Kocha huyo pia amesisitiza
suala la mechi yao ya marudiano ya Kombe la Shirikisho dhidi ya FC Plutnum
kwamba ni muhimu zaidi.
0 COMMENTS:
Post a Comment