April 1, 2015


Beki wa zamani wa Simba, Talib Hilal na kikosi chake cha timu ya taifa ya ufukweni ya Omani, wametoa zawadi ya ubingwa wa Asia kwa Mfalme wa Qaboos wa Oman.

Talib aliyewahi kuichezea na kuifundisha Simba hadi kuipa ubingwa wa Ligi Kuu Bara mwaka 2008, wametoa ubingwa huo kwa Mfalme wao.

Oman wamefanikiwa kuwa mabingwa kwa kuwafunga Japan katika michuano ya Asia ya Ufukweni iliyofanyika jijini Doha Qatar.

Pamoja na ubingwa huo, Talib ameiongoza Oman kupata nafasi ya kushiriki Kombe la Dunia la Ufukweni litakalofanyika nchini Ureno.


Uamuzi wa kutoa ushindi huo kama zawadi kwa Mfalme Qaboos umetokana na namna yeye na serikali yake kujali michezo kwa kiasi kikubwa ukiwemo mchezo huo wa soka la ufukweni.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic