Yanga imepanga kushinda mechi zake tatu
zijazo za Ligi Kuu Bara ili iwe bingwa kabla ya kwenda nchini Tunisia kupambana
na Etoile du Sahel.
Mkuu wa kitengo cha habari cha Yanga, Jerry
Muro amesema wanataka kupambana washinde mechi tatu.
“Lengo ni kushinda tatu zote, ili tukienda
kupambana na Etoile tayari tunakuwa mabingwa,” alisema Muro.
“Tunajiandaa ili tushinde mechi ya kesho
dhidi ya Stand United. Baada ya hapo, ni zamu ya anayefuatia,” alijigamba Muro.
Yanga itapambana na Etoile wiki mbili zijazo
kuwania kusonga mbele katika Kombe la Shirikisho.
Tayari kuna ugumu baada ya Yanga kupata sare
ya bao 1-1 dhidi ya Waarabu hao jijini Dar. Lakini wachezaji wameahidi
kupambana.
0 COMMENTS:
Post a Comment