Kocha wa makipa wa timu za taifa za Oman na
mkufunzi anayetambuliwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), Haroon Amur Al
Siyabi ameendelea kuwanoa makipa wa Simba, leo.
Al Siyabi ameendelea na mazoezi kuwanoa
makipa hao kwenye Uwanja wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Makipa hao akiwemo Ivo Mapunda, wamekuwa
wakifundishwa mbinu mbalimbali za kisasa za ulinzi kwa makipa.
Al Siyabi alikuwa akiwaonyesha mambo kadhaa
ya namna ya kudaka, kuwasoma washambuliaji na nini cha kufanya ili kujilinda
zaidi.
Kocha huyo nguli katika kazi hiyo ya kunoa
makipa, pia amewahi kumnoa kipa wa zamani wa Simba, Juma Kaseja.
Hata hivyo imeelezwa Al Siyabi anatarajia
kuondoka nchini siku mbili sijazo kurejea kwao Oman kuendelea na majukumu
mengine.
0 COMMENTS:
Post a Comment