NGOMA (KUSHOTO) AKITETA JAMBO NA SALEH ALLY 'JEMBE' (KULIA). KATIKATI NI ZUTTAH AKIINGIA KWENYE GARI. |
Mshambuliaji
Donald Ngoma amerejea kwao Zimbabwe kwa ajili ya maandalizi ya siku chache
kabla ya kurejea nchini kujiunga rasmi na Yanga.
Ngoma
ameiambia SALEHJEMBE kwamba atarejea nchini Jumapili na Jumatatu ataanza kazi
rasmi na timu yake mpya.
Mzimbabwe
huyo amesema ameomba ruhusa ya siku nne kwa kuwa alikuwa amesafiri kwenda DR
Congo kwa ajili ya sherehe fupi ya kuchumbia.
SALEH ALLY 'JEMBE' AKIWAAGA ZUTTAH NA NGOMA... |
“Sasa
sikuwa nimefanya maandalizi ya kutosha. Sasa narejea nyumbani, halafu Jumapili
nitakuwa hapa. Nashukuru uongozi wa Yanga kwa kunisikiliza,” alisema.
Lakini
kiungo kiraka Joseph Zuttah “Tetteh” raia wa Ghana yeye anaendelea kubaki
nchini na tayari ameanza kazi na Yanga.
Wawili
hao wamejiunga na Yanga kwa mkataba wa miaka miwili.
0 COMMENTS:
Post a Comment