Mshambuliaji Jamie
Vardy wa Leicester City ni noma, na hakamatiki na sasa ameweka rekodi katika
Ligi Kuu England baada ya kufunga bao katika mechi 11 mfululizo
Vardy amefunga bao hilo
leo wakati timu yake ilipotoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Man United.
Sare hiyo imeshusha
Leicester hadi katika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 28.
Lakini Vardy anaingia
kwenye rekodi ya kufunga mechi 11 mfululizo za Ligi Kuu England na sasa ni kati
ya washambuliaji wanaotikiza England na gumzo duniani kote.
0 COMMENTS:
Post a Comment