Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm amesema hata kama watakuwa na uchovu lakini kikosi chake kipo tayari kwa ajili ya mechi ya Kombe la FA dhidi ya Coastal Union, leo.
Yanga inaivaa Costal Union mjini Tanga katika mechi inayosubiriwa kwa hamu kubwa.
Pluijm amesema, Yanga lazima watakuwa na uchovu wa safari kutoka Misri na baadaye kuunganisha Tanga, lakini wako tayari.
“Mechi ipo hivyo ni lazima tucheze, itakuwa ngumu kwa kuwa ni ya mtoano. Kikubwa tumejiandaa na tunataka kushinda,” alisema.
Kuhusiana na kwamba wanakutana ana Coastal Union ambayo ilikuwa imewafunga katika mechi ya ligi kwenye uwanja huo.
“Nani kasema aliyekufunga mwanzo lazima akufunge tena. Nafikiri tungoje mchezo ukiisha utaona nini kimetokea,” alisema.
0 COMMENTS:
Post a Comment