Katika kile
kinachoonekana sasa hana nafasi kabisa ya kuendelea kuitumikia Manchester City,
kiungo mkongwe Yaya Toure ameondolewa katika kikosi cha timu hiyo
kitakachocheza dhidi ya Steaua Bucharest, kesho Jumanne katika mechi ya kuwania
kufuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Toure ambaye
ana umri wa miaka 33, hayumo katika mipango ya kocha wake mpya Pep Guardiola na
hilo limeonekana kuanzia katika mechi ya kwanza ya msimu huu dhidi ya Sunderland
ambapo hakujumuishwa katika kikosi cha kwanza.
Man City ipo
Romania kwa ajili ya mchezo huo lakini kiungo huyo raia wa Ivory Coast hayumo
hata katika orodha ya wachezaji 18 waliosafiri kwa ajili ya mchezo huo.
Awali
akizungumzia juu ya majaaliwa ya mteja wake, wakala wa Toure, Dimitri Seluk
alisema ana imani kuwa Guardiola atampa nafasi Toure kuthibitisha ubora wake.
Mbali na
Toure wachezaji wengine mastaa ambao hawajasafiri na timu hiyo ni Eliaquim
Mangala, Samir Nasri na Wilfried Bony.
Toure yupo
katika mwaka wa mwisho wa mkataba wake ambapo anaendelea kulipwa mshahara
unaokadiriwa kuwa ni pauni 250,000 kwa wiki na inaonyesha kuwa hana maisha
marefu klabuni hapo.
0 COMMENTS:
Post a Comment