Licha ya
Kocha Arsene Wenger kudai kuwa kipigo cha mabao 4-3 ambacho timu yake ilikipata
jana Jumapili kutoka kwa Liverpool, kimetokana na wachezaji wake kuwa majeruhi
na wengine kutokuwa fiti, mshambuliaji mkongwe wa zamani wa timu hiyo, Thierry
Henry amekosoa mfumo unaotumika ndani ya Arsenal.
Henry
amesema kuwa anashindwa kuelewa kwa nini timu yake hiyo inashindwa kuweka fedha
sokoni kisha ikashindana na timu nyingine kubwa katika kuwania wachezaji wenye
uwezo mkubwa licha ya kutajwa kuwa ni moja ya klabu tajiri.
“Kitu ninachoshindw
akukielewa ni kuwa Arsenal inatajwa kuwa klabu tajiri lakini inashindwa
kushindana sokoni kuwania wachezaji," alisema Henry alipokuwa akizungumzia
juu ya mwenendo wa Arsenal, kisha akaongeza kwa kusema:
"Unadhani
wachezaji wakubwa watavutiwa kuichezea Arsenal? Unadhani klabu ina mifumo ya
kuwavuta? hayo ni maswali unayotakiwa kujiuliza.”
Thierry
Henry ametamka hayo siku chache tangu alipoondoka klabuni hapo na kuachana na
mafunzo ya ukocha aliyokuwa akiendelea nayo klabuni hapo baada ya Wenger
kumtaka achague moja kati ya kuendelea kuwa klabuni hapo kufundisha au kuwa
mchambuzi kwenye uninga.
Kauli hiyo
ni mwendelezo wa lawama nyingi ambazo Wenger amekuwa akitupiwa akionekana ni
mzito kufanya maamuzi ya kusajili wachezaji wakubwa ambapo Henry amesema anaamini
Arsenal bado inahitaji straika mmoja na beki wa kati.
0 COMMENTS:
Post a Comment