October 20, 2017


Kocha mpya wa Simba, Irambona Masoud Juma amezua gumzo mtandaoni baada ya kusema kauli mbalimbali.

Kauli mbili za kuwa hatafunga begi lake na kama mabaya ataondoka zake mapema kurejea Kigali, Rwanda na ile wachezaji wavivu wajiandae, imewavutia watu wengi.

Kutokana na wengi kuvutiwa na kauli hiyo, wamekuwa wakijadili mambo kadhaa ikiwemo kuwachambua wachezaji wavivu.

Lakini baadhi wamekuwa wakieleza kufurahishwa na namna kocha huyo alivyoonyesha kujiamini hiku baadhi wakitaka viongozi na wachezaji wenyewe kumuunga mkono.

Kocha huyo kijana amejiunga na Simba akitokea nchini Rwanda ambako alifanya vizuri na Rayons Sports.

Kabla Masoud alikuwa mchezaji wa APR ya Rwanda ambako alifanya vizuri kabla ya kustaafu na kuwa kocha.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic