January 18, 2018

KOCHA MPYA WA SIMBA, MFARANSA PIERRE LECHANTRE AKIWA NA MHARIRI MKUU WA CHAMPIONI, SALEH ALLY JEMBE BAADA YA KUMFUATA KATIKA HOTELI ALIYOKUWA AMEFICHWA.


Pamoja na juhudi kubwa za Klabu ya Simba kufanya juhudi za kumficha kocha wake mpya Mfaransa, Gazeti la CHAMPIONI limefanikiwa kumuibua mafichoni.

Kocha huyo ametua nchini juzi usiku na uongozi wa Simba umefanikiwa kumficha hadi alipoibuliwa na gazeti hilo.

Kocha huyo anajulikana kwa jina la Mfaransa Pierre Lechantre na anatarajia kusaini mkataba mpya leo.

Lechantre amekuja pia na kocha wa viungo Mmorocco Mohammed Aymen Hbibi.

Kocha huyo mzoefu ataanza kazi mara moja na atasaidiwa na kocha msaidizi wa sasa Masoud Djuma ambae alikuwa akikaimu nafasi hiyo.

Kocha Lichantre keshawahi kufundisha klabu kadhaa duniani kikiwemo kikosi cha Timu ya Taifa ya Cameroun kilichotwaa ubingwa wa Africa 2000.

Kocha huyo pia alipata kuwa kocha bora wa Afrika mwaka 2001 na pia barani Asia mwaka 2012.



1 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic