January 20, 2018



Baada ya mgomo wa muda wa takribani wiki mbili, kipa Beno Kakolanya hatimaye amerejea mazoezini Yanga.

Kakolanya amerejea na kuendelea na mazoezi na wenzake kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam kuendelea kujiandaa na mechi zijazo za Ligi Kuu Bara.

Kipa huyo mzoefu aliyejiunga na Yanga akitokea Prisons ya Mbeya, aliweka mgomo akitaka kumaliziwa fedha alizokuwa anadai.

Hata hivyo, ilionekana uongozi wa Yanga ulikuwa ukipambana kumrejesha Obrey Chirwa ambaye pia aligomea kwao Zambia kutokana na kutolipwa fedha zake pia.


Baadaye, uongozi huo ulifanikiwa kumrekesha Chirwa timu ikiwa kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi na sasa Kakolanya naye amerejea.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic