February 23, 2013





Baadhi ya wachezaji wa Azam FC huenda wakaingia katika mtego wa adhabu kutoka kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) hasa kama kamisaa wa mchezo wao dhidi ya Yanga ataandika kuhusiana na ilivyokuwa.
Mara baada ya mechi yao ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Yanga ambao walilala kwa bao 1-0, wachezaji wa Azam FM walimvamia mwamuzi wa mchezo huo wakimlaumu kwamba muda wa ziada haukuonyeshwa.
Baadhi ya wachezaji wa Azam FC walidiriki kumsukuma mwamuzi huyo ambaye baada ya nusu dakika alikuwa katika wakati mgumu hadi askari polisi walipolazimika kuingia uwanjani kumuokoa.
Hata pamoja na askari hao kuingia uwanjani, bado wachezaji wa Azam FC waliendelea kupandisha jazba wakibishana na baadhi ya askari hao.
Mwisho, askari hao walitoka na mwamuzi huyo akiwa chini ya ulinzi mkali unaokaribia ule anaopewa rais wan chi hasa anapokuwa katika msongamano wa watu wengi.
Lolote linaweza kutokea lakini ripoti ya kamisaa ndiyo inaweza kuwa jibu la mwisho kuhusiana na kilichotokea katika mechi hiyo iliyohudhuriwa na watu wengi zaidi kuliko nyingine tokea mzunguko wa pili ulivyoanza.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic