BAADA ya
kiungo nyota wa zamani wa England, Paul Ince kupewa kazi ya kuifundisha Blackpool,
kitu cha kwanza kilichozua gumzo si kazi yake hiyo badala yake ni mwanaye.
Ince
aliyewahi kung’ara akiwa na Man United na baadaye Inter Milan na Liverpool,
ameingia mkataba wa mwaka mmoja kuinoa Blackpool baada ya kocha wa zamani
kutupiwa virago.
Kinachowavutia
wengi zaidi, Ince aliyekuwa mkorofi wakati wa enzi zake, atakuwa bosi wa mwanaye
Tom Ince ambaye ni mmoja wa wachezaji tegemeo wa Blackpool.
Hata
hivyo, Ince tayari ameonyesha kutotaka ishu ya mwanawe iwe gumzo kubwa zaidi,
badala yake watu waangalie Blackpool inasonga vipi mbele.
Wakati Fulani,
Ince aliwahi kumshambulia kocha wake wa zamani, Alex Ferguson kwa madai alikuwa
akifanya kazi na mwanaye na kutaka kuifanya timu hiyo kama familia.
Ince
ameona mwelekeo wa wadau wengi ni huko, naye amekuwa mwepesi kukumbushia huku
akisisitiza, aachwe afanye kazi yake.
Kuonyesha amepania kuifanya kazi yake vizuri,
Ince ameutaka uongozi wa Blackpool kumbakisha kocha msaidizi, Steve Thompson
ili aendelee naye.
0 COMMENTS:
Post a Comment