May 31, 2013



 
Taarifa zinaeleza mwili wa Mangwea utafanyiwa uchunguzi kwa mara nyingine.

Mmoja wa wafanyakazi wa Hospitali ya St Helen Joseph ya jijini Johannesburg amesema uamuzi huo umetokana na kutokamilika kwa mambo kadhaa baada ya uchunguzi wa kwanza.

“Kuna vitu havikukamilika, lakini kuna mambo tumeona kama si sahihi, hivyo tutachunguza tena,” alisema na alipoulizwa kuhusiana na walichokiona katika ripoti ya kwanza, akajibu:

“Kawaida ndugu zake ndiyo wanatakiwa kupokea ripoti, huenda ikatoka Jumatatu. Hivyo watapewa watu wanaohusika.”

Mmoja wa Watanzania anaoishi Afrika Kusini, amesema wamekuwa na hamu kubwa ya kutaka kujua kilichomuua Mangwea kwa kuwa taarifa zimekuwa ni za kutatanisha.

“Kweli kila mtu anataka kujua, tatizo linakuwa ni moja kwamba mambo yanakwenda kwa siri sana.

“Lakini hata kati yetu huku kuna watu wamekata tama kwa kuwa haijulikani mambo yanakwenda vipi.
 
“Lakini kuna wengine wanaendelea kuchanga, mfano kuna daftari linapita huku Hillbrow na kwingine na watu wanaendelea kuchanga.
“Awali tuliambiwa serikali imechukua jukumu, lakini baadaye wanasema Clouds ndiyo watafanya mambo yote. Sasa kiasi Fulani tunakuwa hatuelewi kinachoendelea,” alisema Mtanzania huyo anayeitwa Joseph.
Mwili wa Mangwea bado uko katika chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya St Helen Joseph.
Taarifa zinaeleza mwili huo utaondoka huko Jumapili mchana na kuwasili jioni kwa kuwa kwa ndege ni mwendo wa saa tatu na nusu.
Kuagwa kwake itakuwa Jumatatu kuanzia saa 3 asubuhi na baada ya hapo atasafirishwa kwenda Morogoro kwa mama yake ambako atapumzishwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic