July 10, 2013



 
M TO THE P AKIPEWA MKONO NA RAIS KIKWETE

MWINA KADUGUDA NAYE AKIPEWA MKONO...

Wasanii na wanamichezo mbalimbali walionyesha wenye wako ‘shap’ ili kufanikiwa angalau kupata mkono salamu kwa kusalimiana na Rais Jakaya Kikwete.

Hali hiyo ilitokea wakati wa Tamasha la Matumaini mwishoni mwa wiki iliyopita wakati Rais Kikwete akishuka jukwaani kwenye uwanjani kukagua timu za Wabunge wa Yanga na Simba.
 
MANYIKA FULL TABASAMU...

JB AKIMWAGA 'SERA'..

Kwa kuwa wasanii wa Bongo Movie na Bongo Fleva hawakuwa katika programu ya kumsalimia Rais Kikwete, ‘fasta’ walitengeneza mstari wao na kumvizia akiwa njiani kwenda uwanjani.

M To The P, rafiki mkubwa wa marehemu Albert Mangweha ‘Ngwea’ alikuwa kati ya wasanii wa kwanza wa Bongo Fleva waliomsalimia Rais Kikwete na kufuatiwa na wengine kama Manyika Peter akiwemo nahodha wao H Baba.

Lakini JB na Dk Cheni waliowaongoza Bongo Movie pia kusalimia na Rais Kikwete.

Katibu Mkuu za zamani wa Simba pia Fat, Mwina Kaduguga pia alionyesha ni ‘shap’ kinoma, baada ya kufanikiwa kusalimia na rais huku wakizungumza “mawili matatu”.

Karibu kila aliyepata bahati hiyo alionekana ni mwenye furaha kupindukia.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic