February 5, 2014




Pamoja na kurejea kikosini, kiungo nyota Athumani Iddi ‘Chuji’ hatacheza katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Komoronize ya Comoro.


Chuji alipata kadi ya nyekundu katika mechi dhidi ya Zamalek ya Misri wakati Yanga ikishiriki Ligi ya Mabingwa Afrika, mwaka juzi.
Chuji ambaye amerejea Yanga baada ya kusimamishwa muda usiojulikana tayari yuko kambini Bagamoyo.

Habari za Chuji kukosa mechi hiyo zimethibitishwa na msemaji wa Yanga, Baraka Kizuguto.
Alijiunga na kikosi hicho na tayari kocha Hans van Der Pluijm ameonyesha kuikubali kazi yake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic