February 5, 2014





Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na Klabu ya Yanga zimeendelea kuvurugana kuhusu kama Yanga ni halali kumtumia mshambuliaji Emmanuel Okwi katika mchezo wa Klabu Bingwa Afrika dhidi ya Comoronize utakaopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar wikiendi ijayo.
 
Okwi yupo katika wakati mgumu baada ya TFF kusimamisha usajili wake huku ikitaka kupata ufafanuzi kutoka Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) kama ni halali Wanajangwani hao kumtumia au la.

Okwi awali alikuwa mchezaji wa Simba aliyeuzwa kwenye kikosi cha Etoile du Sahel lakini baadaye aligoma kwa kuwa hajalipwa mshahara na kusajiliwa kwa mkopo na SC Villa ambayo ilimuuza kwa Yanga.

Akizungumza na Championi Jumatano, Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Seif Magari, alisema kuwa tayari wameshamuandaa mchezaji huyo kwa ajili ya kumtumia katika mchezo wa Jumamosi dhidi ya Comoronize, lakini bado hawajapata barua kutoka TFF hadi sasa.
“Tumemuandaa vyema Emmanuel Okwi kwa ajili ya mchezo wetu dhidi ya Comoronize tutakaocheza Jumamosi kwani yupo safi na amejiunga na wenziye na kiwango chake kinaonekana kipo juu.
“Tunawasubiri TFF waweze kututaarifu kwa barua kama tunaweza kumtumia Jumamosi lakini hadi sasa hakuna barua yoyote tuliyoipata ambapo tunasubiri jibu lao,” alisema Magari.
Aidha kwa upande wa TFF kupitia kwa Ofisa Habari wake, Boniface Wambura, amefunguka kuwa: “Okwi tumemfungia leseni ya kucheza ligi kuu hivyo iwapo mchezaji hana leseni ya kucheza ligi ya ndani haruhusiwi kucheza mechi za kimataifa na kwa sasa tunasubiri barua kutoka Fifa ambayo itatoa maamuzi.”

Yanga wana matumaini kuwa wanaweza kupewa ruhusa ya kumtumia mshambuliaji huyo kwenye mchezo wa wikiendi ijayo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic