February 7, 2014





Na Saleh Ally
KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger si mtu mwenye mambo mengi, vituko au mbwembwe na hana rekodi ya kuwa na wachezaji wenye vituko.


Taarifa za kwamba anavutiwa na uwezo wa mshambuliaji wa zamani wa Manchester City, Mario Balotelli zimeonyesha kuwashitua wengi, lakini yeye ameendelea kuwa kimya.

Wenger amekuwa kimya lakini tayari taarifa zimevuja kwamba wadhamini wao wapya wa vifaa, Kampuni ya Puma ya Ujerumani, wameahidi kufanya kila linalowezekana kuhakikisha mtukutu huyo anatua Emirates.

Uongozi wa Arsenal umekaa kimya kuhusiana na suala hilo la juhudi za kumtoa Balotelli kutoka AC Milan na kumrejesha England akipige katika klabu yao ya Arsenal.


Hiyo ni dalili kuwa kweli Wenger anamhitaji Balotelli kwa ajili ya kuimarisha kikosi cha kwanza msimu ujao, iwe ametwaa ubingwa au la.

Hawezi kuwa mjinga kwa kujishusha kwa Balotelli, muhimu kwake ni mafanikio, ndiyo maana Alex Ferguson aliwahi kusafiri hadi Ufaransa kumbembeleza Eric Cantona aliyekuwa amevuruga na baadaye kurejea kwao kwa kiburi.


Kawaida makampuni yote yanayodhamini, hupenda kuona sehemu wanayoingiza fedha zao kunakuwa na mafanikio makubwa ili kuwatangaza wao zaidi.


Kwa kuwa Arsenal wameonyesha wanamhitaji Balotelli, Puma wanaamini kama atajiunga na Arsenal, macho na masikio kwa wingi zaidi yataelekezwa kwa timu hiyo na kuwasaidia wao kujitangaza zaidi.

Lakini taarifa nyingine zinaeleza hizo zilikuwa juhudi za Puma kutaka kumshawishi Balotelli kuingia upande wao na kuachana na Nike mara tu mkataba wake ulipomalizika, ambapo tayari amejiunga na Puma.

Puma wamefanikiwa kuing’oa Nike katika kikosi cha Arsenal baada ya kutoa mkataba mnono zaidi ikiwa ni katika kampeni zao za kurudi kwenye chati ya juu hasa katika soka.

Utukutu:
Inaonekana Wenger hana rekodi ya kuwa na wachezaji watukutu kama ilivyo kwa Balotelli ambaye ana tabia za kupigana hadi na wenzake mazoezini.

Wakati fulani, aliyekuwa Kocha Mkuu wa Man City, Roberto Mancini, alilazimika kumkwida kwa kuwa alionekana si muelewa.

Kazi ambayo Wenger hawezi kuifanya hata iwe vipi na swali ni kama Balotelli atakuwa amebadilika maana tangu alipoondoka England, tayari katika umri wake mwaka mmoja umeongezeka.

Tafrani:
Achana na kuwa mgomvi, vituko vingine vya Balotelli ni kuonekana kwenye klabu za usiku hata siku moja kabla ya mechi.

Ukali wa Mancini kiasi fulani ulichangia kupunguza, wataalamu wa masuala ya soka nchini England, wanasema Wenger ni kati ya makocha wakali huenda kuliko wote na hataki mchezo.

Kama ni hivyo, basi haitakuwa kazi ngumu kukabiliana na tafrani hizo za Balotelli ambaye anajulikana kwa kipaji na utukutu.

Kiwango:
Kiwango chake kimeporomoka, hizi ni hisia za wengi lakini kwa ufuatiliaji mzuri na majibu ya takwimu zake zinaonyesha bado moto wake ni uleule.

Huenda ndiyo maana Wenger ‘amenusa’ kama ilivyo kawaida yake na kuamua kuweka kando utukutu wake na kuangalia kazi yake.

Msimu wa 2011-12 alicheza mechi 40, hapa ni zile za Ligi Kuu England alizochezea kikosi chake cha Man City. Kati ya hizo 25 alianza na 15 kuingia na alifanikiwa kufunga mabao 19.

Msimu wa  2012-13 alicheza mechi 45, kati ya hizo 31 alianza na 14 aliingia na hadi mwisho pamoja na timu ya taifa, alifanikiwa kufunga mabao 23.

Pamoja na kuuanza vizuri msimu huu, wakati unakwenda ukingoni mambo yanaonekana si shwari sana kwake. Maana amecheza jumla ya mechi 31, kati ya hizo sita akiwa ameingia na tayari ana mabao 18.

Yote yanawezekana, kikubwa hapa ni kusubiri kipindi cha usajili kikianza, halafu tutaona.

Takwimu za msimu huu kwa klabu:
MECHI 16
MABAO 9
PASI ZA MABAO 3
MASHUTI 99
Fin.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic