February 7, 2014





Baadhi ya wanaodaiwa kuwa ni viongozi wa Azam TV, juzi walizua varangati baada ya kutokea mvutano kati yao na vyombo vingine vya habari vilivyokuwa vikirekodi katika video mechi ya Ligi Kuu Bara kati ya Mtibwa Sugar na Simba kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.


Awali wapiga picha mbalimbali waliweka mitambo yao sawa na kuanza kurekodi baadhi ya matukio kabla ya mechi hiyo, lakini baada ya muda wahusika wa Azam TV waliwavaa na kuwaamuru waache kurekodi.

Alipofuatwa mmoja wa mabosi wa Azam TV ambaye hakutaja jina lake, alisema walisahau kutoa taarifa mapema juu ya taratibu zilizopo sasa kwa kuwa wao ndiyo wenye mamlaka ya kurekodi michezo hiyo katika video.

“Hawakujua taratibu zetu, ila tumebahatika kuwazuia, anayetaka matukio muhimu lazima afuate taratibu, hatuna kipingamizi cha kuwapatia,” alisema.

Azam TV ndiyo yenye mkataba na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) wa kurekodi na kuonyesha mechi za ligi hiyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic