February 5, 2014





Klabu ya Yanga imetangaza rasmi vituo kumi vitakavyouza tiketi la pambano lao la Klabu Bingwa Afrika dhidi ya Komorozine ya Visiswa vya Comoro itakayopigwa Jumamosi ya wiki hii kwenye uwanja wa Tiafa jijini Dar.
 
Ofisa Habari wa Yanga, Baraka Kiziguto amesema wamechapa tiketi 45,000  kwa ajili ya mashabiki wake na wataanza kuziuza keshokutwa Ijumaa kupitia vituo vya:

Sokoni Kariakoo, Oil Com- Buguruni, Dar Live, Uwanja wa Uhuru, Steeaz Samora, Oil Com Ubungo, Kimara mwisho, Mwenge stendi, Shule ya Benjamini Mkapa na basi maalum ambalo litakuwepo klabuni.

Viingilio vitakuwa kama ifuatavyo: VIP A 30,000 ( tiketi 500), VIP B&C 20,000 (4500), Orange 10,000 (7000) na viti vya Bluu na kijani 5000 (33,000). 
Aidha alisema wapinzani wao wanatarajia kuwasili leo Jumatano kupitia shirika la ndege la Air Tanzania na kesho watafanya mazoezi kwenye uwanja wa Karume na Ijumaa watahamia uwanja wa Taifa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic