February 5, 2014




Uongozi wa klabu ya Yanga ni kama umeonyesha hofu ya kumtumia au kutomtumia mshambuliaji Emanuel Okwi kwenye mechi ya Jumamosi dhidi ya Wacomoro kwa kuwa mpaka sasa hawajapata taarifa kutoka TFF kama wanaweza kumtumia.
 
Awali Okwi alizuiwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) wakidai mpaka wajiridhishe Fifa kama Yanga wanapaswa kumtumia mchezaji huyo aliyejiunga akitokea Sports Club Villa ya Uganda.

Ofisa Habari wa Yanga Baraka Kizuguto amesema mchezaji huyo licha ya kuwa amepitishwa na Shirikisho la Soka la Afrika Caf lakini wao wanasubiri tamko kutoka TFF ambao nao wanasubiri majibu kutoka Fifa.

“Tunachosubiri ni kupewa ‘go a head’ kutoka TFF, lakini mchezaji wetu amepitishwa na Caf kuichezea Yanga kwenye michuano hiyo kwa kuwa tulimsajili kwa kufuata kanuni zote na ITC tukapata,” alisema Kizuguto na kuongeza:

“Tumepewa taarifa na Caf kutukumbusha tusimtumie kiungo wetu Chuji kwa kuwa katika mchezo wa mwisho alipata kadi nyekundu dhidi ya Zamalek.” 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic