March 15, 2014


Kipa namba moja wa Yanga, Deogratius Munish ‘Dida’ ameumia mkononi ingawa haijajulikana sababu ni nini.

Dida ameweka picha kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook inayoonyesha jeraha ambalo limepatiwa matibabu na kusema kuwa ameumia.
PICHA ALIYOWEKA
Kutokana na hali hiyo, wakati Yanga ikiivaa Mtibwa Sugar leo, kipa Juma Kaseja alishika nafasi hiyo ya Dida huku benchi akikaa Ally Mustapha ‘Barthez’ ambaye sasa ni kipa namba tatu.

 Dida ndiye amekuwa kipa chaguo la kwanza tokea Kocha Hans van Pluijm alipotua nchini na kuanza kuinoa Yanga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic