March 23, 2014




Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic amesema mechi ya leo dhidi ya Coastal Union ni kama vile mtihani wa mwisho kwa mwanafunzi.

Logarusic ameiambia SALEHJEMBE kwamba anaamini kama watapotea katika mechi dhidi ya Coastal Union, basi nafasi mbili za ubingwa na ile ya pili zinaweza kuwa ngumu kwao.

“Lazima kushinda Jumapili (leo) dhidi ya Coastal, kama tutapoteza basi tutakuwa tumejiondoa kabisa kwenye ubingwa na kuchukua nafasi ya pili.

“Mechi itakuwa ngumu lakini tuna kila sababu ya kushinda kwa kuwa tuna kikosi kizuri na chenye uwezo,” alisema Logarusic.
Simba iko katika nafasi ya nne ikiwa na pointi 36 nyuma ya Azam FC, Yanga na Mbeya City ambazo zinazidi kuchanja mbuga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic